Download | Play Now

AUDIO | Mbosso – Nusu Saa | Download

Baada ya mafanikio ya wimbo wake wa kwanza “Pawa”, msanii kipenzi cha mashabiki Mbooso amerudi tena na ngoma mpya ya pili kutoka kwenye EP yake yenye jumla ya nyimbo 7, chini ya lebo ya KhanMusic. Ngoma hii inakwenda kwa jina la “Nusu Saa” – na ni mwendelezo wa simulizi la mapenzi ya dhati.

Katika “Nusu Saa”, Mbooso anaendelea kumwimbia mpenzi wake kwa hisia na mahaba tele, akisisitiza kuwa muda hautoshi kuelezea mapenzi yake:

“Imetosha tangu nikupate wewe,
Robo saa haitoshi,
Nusu saa, hata masaa – hatoshi kusema na wewe…”

Mashairi haya yanagusa moyo na kuonyesha jinsi mapenzi ya kweli yanavyokuwa na kina. Mbooso anaongeza upole na kujitoa kwa mpenzi wake kwa kusema:

“Deka kama unavyodeka kama mtoto,
Nitakukubembeleza – mimi ni wako.”

Mbooso Nusu saa

Kama ilivyokuwa kwenye “Pawa”, pia hapa Mbooso anaonyesha ubunifu wa hali ya juu, akiwa amepangilia mashairi kwa uangalifu, beat laini yenye ladha ya Bongo Flava na Afro-RnB, huku production ikiwa safi na ya kiwango cha juu.

Download “Nusu Saa” – Mbooso (MP3)

📥 Bofya hapa chini kudownload wimbo “Nusu Saa”

Download | Mbosso – Nusu Saa [Mp3 Audio]

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *